Rais Jakaya Mrisho Kikwete amekemea vikali vurugu zilizotokea jana mkoani Mtwara baada ya kusomwa bungeni kwa Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.
Akizungumza katika
eneo la Kizota mkoani Dodoma wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa
Barabara ya Dodoma kwenda Iringa, Rais Kikwete alisema wote waliohusika na
vurugu hizo watasakwa na kuchukuliwa hatua kali.
Rais Kikwete alisema
rasilimali inayopatikana mahali popote pale nchini inatakiwa kutumiwa na
Watanzania wote.
“Hivi watu wa Nyarugusu wadai dhahabu ya pale au
kinachopatikana Chalinze basi kisitumiwe na watu wa Morogoro! Hivi tutakuwa na
taifa kweli?,” alihoji kwa ukali Rais Kikwete.
Rais Kikwete
alisisitiza kuwa Serikali itawasaka wale wote wanaoongoza vurugu hizo na
watawajibishwa kwa makosa hayo.
“Tutawasaka hawa watu na viongozi wao hata kama wana mapembe
kiasi gani, tutayakata.” Alisema kwa msisitizo
No comments:
Post a Comment