Saturday, January 26, 2013

Mmea wa kukuza sehemu za siri wagundulika

 Kwa ufupi

Katika mitaa ya miji na majiji nchini, siyo jambo la ajabu kukutana na mabango hayo, ambayo hata hivyo kushamiri kwake kunaleta picha kwamba ni kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo nchini, huku watoa huduma husika wakinufaika kwa kujikusanyia kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa wahitaji.
 
 
KWA kutumia mabango, lengo likiwa kutangaza kazi zao, waganga wengi wa tiba asilia wamekuwa wakijinadi kuwa wanatoa tiba ya kurefusha maumbile ya siri ya wanaume, kukuza makalio au matiti.

Katika mitaa ya miji na majiji nchini, siyo jambo la ajabu kukutana na mabango hayo, ambayo hata hivyo kushamiri kwake kunaleta picha kwamba ni kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo nchini, huku watoa huduma husika wakinufaika kwa kujikusanyia kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa wahitaji.

Pia dawa zinazodaiwa kukuza makalio maarufu kama ‘mchina’, zimekuwa gumzo baada ya kuingia nchini, huku zikielezwa kukosa ubora na kwamba zina madhara makubwa.

Lakini, sasa unaweza kuachana na dawa hizo za Kichina, baada ya kugundulika mmea wenye uwezo wa kukuza makalio, matiti, pamoja na kurefusha uume.

Taarifa za kiutafiti zinautaja mti huo kwa jina la Mvunge, ukiwa na uwezo wa kukuza makalio, matiti na kurefusha uume.

Kaimu Msajili wa Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini, Dk Naomi Mpemba anasema kuwa mmea huo ambao huwa ni mti mkubwa upo na kwamba una uwezo mkubwa wa kukuza maumbile hayo.

Anabainisha kuwa mmea huo ambao hukua na kuwa mti mkubwa huzaa matunda yanayotumika kama dawa na unapatikana wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga, Pwani, Mbeya, Morogoro na baadhi ya mikoa nchini.

“Tulifuatilia na kutambua kuwa mti huo upo maeneo hayo na unatumiwa zaidi na waganga, hata picha za mti huo tunazo,” anasema Dk Mpemba na kuongeza:

“Jina jingine unaitwa Miegeya, mara nyingi unastawi katika maeneo yenye ardhi ya unyevunyevu, una tabia ya kustawi kama Mwembe na matunda yake huonekana kufanana na Mbuyu.”

Hata hivyo, anasema kuwa asilimia kubwa ya waganga wa tiba asili na tiba mbadala wanaotumia dawa hiyo ni wale wasiokuwa na usajili kutoka baraza hilo, hivyo kufanya huduma hizo kinyume cha utaratibu.

“Kwa mujibu wa masharti yaliyopo katika agizo la Serikali kwa waganga hao, miiko, maadili na utendaji wa kazi zao umeelekeza kuwepo na usiri na kuaminiwa, kwa hiyo sisi tunaamini wanaojitangaza kutibu mambo hayo ni matapeli,”anasema Dk Mpemba.

No comments:

Post a Comment