Thursday, March 28, 2013

MBUNGE WA UVCCM (CCM) ARUSHA ATOA MISAADA YA KIJAMII KWA WAGONJWA NA WATOTO YATIMA JIJINI ARUSHA MACHI 29,2013

 
Mbunge wa Viti Maalum,kupitia UVCCM (CCM) mkoani Arusha Bi. Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akimkabidhi  Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Frida Mokit msaada wa mablang’eti ya kujifunikia wagonjwa waliolazwa Hospitalini hapo.
 
Taasisi ya Maendeleo isiyo ya kiserikali ya Catherine Foundation ya jijini Arusha Machi,28,2013 imetoa misaada mbalimbali ya vyakula kwa wagonjwa Hospitali ya Mt Meru na vituo viwili vya Yatima vya Faraja na Lohada Moshono vyote vya jijini humo.



Mbunge wa Viti Maalum wa UVCCM (CCM), Catherine Magige ambaye ni Kiongozi wa Taasisi ya Catherine Foundation, akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Mt. Meru ya jijini Arusha na kuwapa zawadi mbalimbali.


Misaada hiyo ya vyakula na sabuni pamoja na kuwatembelea wagonjwa kufanyika ikiwa ni sehemu ya kuwapa faraja wagonjwa na yatima hao wakati huu wa kuelekea sikukuu ya Pasaka ili nawao wajisikie ni miongoni mwa jamii.

No comments:

Post a Comment