Friday, March 1, 2013

HEKARI 150 ZA MADAWA YA KULEVYA AINA YA BANGI ZATEKETEZWA ARUSHA RPC AONGOZA OPERESHENI,VIROBA 32 VYAPATIKANA

Na Rashid Nchimbi wa jeshi la PolisiArusha
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=9aaa785771&view=att&th=13d27e0032690299&attid=0.2&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9nc06gubqG_9TDkvcs6-Nb&sadet=1362198246102&sads=7mhIFZ7ViyEbs49T5H6rd41lpqg&sadssc=1
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas akishirikiana na askari wa jeshi hilo kuharibu mimea ya madawa ya kulevya aina ya bangi kwa kuikata kata kisha kuichoma moto katika operesheni iliyofanyika wilayani Arumeru (Picha na Rashid Nchimbi wa jeshi la polisi Arusha)
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=9aaa785771&view=att&th=13d27e0032690299&attid=0.3&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9nc06gubqG_9TDkvcs6-Nb&sadet=1362198250648&sads=qRxKb8Tkzp5dYGYRnur_YpYLznc
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas akibeba begani mimea aina ya bangi tayari kwa kuikusanya kwa pamoja na kisha kuichoma moto katika operesheni iliyofanyika wilayani Arumeru. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=9aaa785771&view=att&th=13d27e0032690299&attid=0.4&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9nc06gubqG_9TDkvcs6-Nb&sadet=1362198255507&sads=YvZ-iO_JdLL3V6vmYrpXe95uRic
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas akichoma moto baada ya kuikusanya kwenye kundi
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=9aaa785771&view=att&th=13d27e0032690299&attid=0.5&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9nc06gubqG_9TDkvcs6-Nb&sadet=1362198259920&sads=KR6KmxSwhAgTPU3cPmJRyY1PNV8
Askari wakipakua viroba vya madawa ya kulevya aina ya bangi toka kwenye gari aina ya defender/Land Rover na kupakia kwenye gari kubwa aina ya Scania mara baada ya kukusanya toka katika maeneo ya mashambani ambapo mizigo hiyo ilifichwa. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=9aaa785771&view=att&th=13d27e0032690299&attid=0.6&disp=inline&safe=1&zw&saduie=AG9B_P9nc06gubqG_9TDkvcs6-Nb&sadet=1362198267566&sads=MK0fxuXTMekzN5kCevKCLSzIhpg
Askari wa Jeshi la polisi kutoka vikosi mbalimbali wakiwa wanapanga mikakati kabla ya kuingia katika mashamba yaliyowazunguka kuharibu madawa ya kulevya aina bangi na kisha kuiteketeza kwa moto 
 katika operesheni iliyofanyika wilayani Arumeru. 
(Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)


Jeshila Polisi mkoani hapa kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Usalama limefanikiwa kuteketeza mimea aina ya bangi iliyokuwa imeoteshwa kwenye mashamba yanayokadiriwa kuwa na ukubwa wa hekari 150 kwenye vijiji viwili tofauti vya Likamba na Imbibya ngalaoni vilivyopo wilaya ya Arumeru.

Operesheni hiyo iliyokuwa inaongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas ilianza mapema asubuhi siku ya tarehe 01.03.2013 kwa askari hao kuingia katika mashamba mbalimbali yaliyopo katika vijiji hivyo.

Mara baada ya kufika wilayani hapo askari hao walianza kuingia katika kijiji cha Likamba na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wakiwa na viroba kadhaa vya bangi na kisha kuhamia kijiji jirani cha Imbibya Ngelaoni ambapo mbali na kuendeleza operesheni ya utafutaji wa viroba vya madawa hayo lakini pia jeshi hilo lilifanikiwa kuharibu mimea ya madawa hayo kwa kuifyeka na kisha kuiteketeza kwa moto.

Viroba vingi vya madawa hayo vilionekana vimefichwa katika mashamba yaliyokuwa yameoteshwa mahindi huku wenyeji wa maeneo hayo wakiyahama makazi yao kwa muda na kukimbilia milimani.

Akizungumza katika eneo la tukio Kamanda Sabas alisema jumla ya viroba vilivyopatikana ni 32 vyenye uzito tofauti huku watuhumiwa watatu ambao ni JaluoTendevesi (32) na Tikayo Kilamee (23) wote wawili ni wakulima na ni wakazi wa kijiji cha Ndevesi wilayani Arumeru pamoja na Ngwerenya Siraitei (55) Mkulima Mkazi wa Mombo mkoa wa Tanga walikamatwa.

Kufuatia mafanikio hayo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Kamishna Msaidiziwa Polisi Liberatus Sabas alitoa shukrani zake kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Stanslaus Mulongo kwa ushirikiano wake mkubwa ambapo ameweza kuunganisha vyombo vya Usalama mkoani hapa na kufanikiwa kutekeleza operesheni hiyo.

Kamanda Sabas alitumia fursa hiyo kuwaomba Wataalamu wa kilimo kuwatembelea wakazi wa maeneo hayo kwa lengo la kuwapa elimu ya kilimo mbadala ili ardhi hiyo waitumie kwa kulima mazao mengine ya chakula na biashara badala ya kuendelea na kilimo cha madawa hayo haramu kwa afya ya binadamu.

Mafanikio hayo ni muendelezo wa ushirikiano mzuri baina ya jeshi hilo na vyombo vingine vya usalama pamoja na wananchi ambao kwa kiasi kikubwa wanatoa taarifa zinazohusu uhalifu na wahalifu kwa jeshi hilo mara kwa mara.

Kwa takriba miezi miwili, Januari na Februari 2013 jeshi hilo limefanikiwa kukamata madawa ya kulevya aina ya Mirungi viroba 372 vikiwa vinasafirishwa toka nchi jirani ya Kenya kuingia nchini na pia madawa ya kulevya aina ya bangi  magunia yapatayo 143 huku kesi za matukio hayo zikiwa zimeshafikishwa mahakamani.

No comments:

Post a Comment