Wednesday, March 6, 2013

SAFARI YA MWISHO YA MJUMBE WA BARAZA KUU UVCCM BENSON MOLLEL

by Pamela Mollel
 Clip 4
Viongozi wa Dini (Wachungaji) wakifanya maombi ya mwisho kabla ya kuuhifadhi mwili wa aliyekuwa Mjumbe  wa baraza kuu la umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), ngazi ya Taifa  kupitia Mkoa wa Arusha, Benson Mollel (26) aliyeaga dunia hivi karibu
 
 Clip 5
Baadhi ya Viongozi walio hudhuria mazishi ya Mjumbe  wa baraza kuu la umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), ngazi ya taifa  kupitia mkoa wa Arusha, Benson Mollel (26) aliyeaga dunia hivi karibu katika hoteli ya Lush Garden Bussines Hotel iliyopo barabara ya vijana mkabala na  Jacaranda  mtaa wa Haile Selassie katikati ya jiji la Arusha
Clip 10
Clip 16
Clip 22
Mama Mzazi wa Marehemu Benson Mollel akiwa analia kwa uchungu baada ya kuweka shada la maua juu ya kaburi la mwanaye
Clip 25
Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas akiwa anatoa heshima za mwisho mara baada ya kuweka shada la maua

Clip 34
Naibu waziri wa nishati na madini Steven Masele katikati aliye valia nguo ya kijani na miwani akishuudia mazishi ya Benson Mollel


Clip 35
Clip 38
Mfanya biashara wa madini maarufu jijini Arusha Bw. Mathias Manga akiwa na Mkewe wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Benson Mollel

Clip 40
Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa jimbo la Monduli Mh.Edward Lowassa akiwa amebeba shada la mau kabla ya kuweka kaburini.


Maelfu ya wananchi wakiwemo viongozi mbalimbali wa kitaifa, viongozi wa dini, vyama vya siasa walijitokeza kumzika aliyekuwa Mjumbe  wa baraza kuu la umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi(Uvccm),ngazi ya taifa  kupitia mkoa wa Arusha ,Benson Mollel (26)aliyeaga dunia hivi karibu katika hoteli ya Lush Garden Bussinnes Hotel iliyopo barabara ya vijana mkabala na  Jacaranda  mtaa wa Haile Selassie katikati ya jiji la Arusha.

Viongozi walioudhuria msiba huo jana nyumbani kwa marehemu katika kata ya Lemara jijini Arusha ni pamoja na Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa jimbo la Monduli Mh.Edward Lowassa, Naibu waziri wa ardhi nyumba na makazi Godluck Ole medeye, Naibu waziri wa nishati na madini Steven Masele, Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo, Mstahiki Meya wa jiji la Arusha Gaudence Lyimo pamoja na viongozi mbalimbali wa UVCCM Taifa na Mkoa.

Msiba huo ulikuwa wa aina yake kutokana msururu wa magari pamoja  na umati mkubwa  wa watu kufika hali iliyopelekea wananchi  wengine kushindwa hata kuaga mwili wa marehem kutokana na ufinyu wa eneo hilo

Katika salamu za rambirambi Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha Robinson Meitenyiku alisema kuwa marehemu ameacha pengo kubwa sana kwana UVCCM na hata kwa wananchi huku akiwataka vijana kumrudia Mungu kutokana na vijana wengi kufa kwa umri mdogo hali ambayo inapelekea nguvu kazi ya taifa kupungua.

“Benson alikuwa mjumbe wa baraza mkoa,kamati ya utekelezaji mkoa na mjumbe wa baraza Taifa tunajua alikuwa na malengo gani na ndiyo tutaenda kuyafanya kwasababu alikuwa ni kiongozi mpenda maendeleo katika jamii”Alisema Meitenyiku

Hata hivyo aliweka wazi kwa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete kuwa toka aingie madarakani pamoja na marehemu hakujawahi kuwepo na makundi katika UVCCM mkoa wa Arusha
“Tunamshukuru Rais kwa salamu zake ila ajue kuwa toka Robinson na Benson waingie madarakani hatujawahi kuwa na makundi ya aina yeyote ile hivyo ushindi uko pale pale”alibainisha  Meitenyiku
Kwa upande wake Naibu waziri wa ardhi nyumba na makazi Goodluck ole Medeye aliwataka vijina kutokukata tama pamoja na kuzingatia elimu inayotolewa na viongozi wa dini,serikali ili kuepuka uvunjifu wa amani hapa nchini.

“Marehemu alikuwa ni mfano mzuri wa kuigwa kutokana na alipenda amani…..Nilipopata taarifa kuwa Benson amefariki nilijiwa na picha ya mgomba mchanga uliyochipua ulipokaribia kuchanua ukakatwa ghafla …..matunda ambayo tulitarajia kuyapata katika mgomba huo hatujayapata “alisema

Aidha aliwakumbusha vijana mshikamano pamoja na upendo miongoni mwao huku akiwataka watumie ujuzi walionao katika kuliendeleza Taifa na kuondoa umaskini.

No comments:

Post a Comment